Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUMTAFUTA MUNGU KATIKA NYAKATI ZENYE KUCHUKIZA!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumatatu Agosti 4, 2025
Juma la 18 la Mwaka

Hes 11:4-15;
Zab 81: 11-16 (K) 1;
Mt 14: 13-21.


KUMTAFUTA MUNGU KATIKA NYAKATI ZENYE KUCHUKIZA!

Leo tunasikia juu ya Yesu kwenda sehemu ya faragha, na kuwalisha watu. Kifungu kimetuchukuwa mbali kutoka katika tukio la kifo cha Yohane Mbatizaji kilicho sababishwa na Herode. Kupanda katika chombo yeye mwenyewe, anakwenda mpaka sehemu tulivu ili kupata muda wa kufikiri….kutafakari na kupata nguvu.

Yesu anachagua sehemu iliyojitenga sio kwa lengo la kujificha bali kuzishughurikia huzuni zake na kutafuta nguvu kwa nyakati zenye kuchukiza. Kujiweka katika sehemu iliyojitenga, sehemu yenye ukimywa hivyo ndivyo tunavyopaswa kufanya wakati tunapohangaika na Imani, na maisha kwa ujumla, na katika huzuni kwa ujumla. Huko ndiko tunakokwenda kulia, kupiga kelele, kupotea, na kutafuta majibu. Kupata jibu katika maswali haya haitoshi tu kuwa pekee katika sehemu iliyojitenga; lakini muhimu zaidi lazima kuwepo kutaniko na Mungu na sehemu iliyojaa uwepo wa Mungu.

Sehemu ya pili kwa asilimia fulani inahusiana na sehemu ya kwanza. Yesu, anayaona mahitaji ya watu na husikia kilio chao. Hakuna mtu aliyeondoka bila ya kushibishwa. Mungu yupo zaidi tunapohangaika. Je, nipo katika jangwa nikitafuta majibu?

Sala: Bwana, njoo katika msaada wangu. Amina.

Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, JUMATATU, AGOSTI 4, 2025




MASOMO YA MISA,
JUMATATU, AGOSTI 4, 2025
JUMA LA 18 LA MWAKA


SOMO 1
Hes. 11 :4-15

Wana wa Israeli walilia wakasema, N’nani atakayetupa nyama tule? Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu; lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu cho chote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hi; mana tu.

Na hiyo mana ilikuwa mfano wa chembe za mtarna, na kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwake bedola. Watu wakazunguka-zunguka na kuikusanya, kisha wakaisaga kwa mawe ya kusagia, au kuitwanga katika vinu, kisha wakaitokosa nyunguni, na kuandaa mikate; na tamaa yake ilikuwa kama tamu ya mafuta mapya. Umande ulipoyaangukia marago wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao.

Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za Bwana zikawaka sana; Musa naye akakasirika.

Musa akamwambia Bwana, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu? Je! ni mimi niliyewatungisha mimba watu hawa wote? je! ni mimi nilivewazaa, hata ikawa wewe kuniambia, Haya, wachukue kifuani mwako, mfano wa baba mwenye kulea achukuavyo mtoto aamwaye, wende nao mpaka nchi uliyowaapia baba zao? Nipate wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? kwani wanililia, wakisema, Tupe nyama, tupate kula. Mimi siwezi kuwachukua watu hawa wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda. Na kama ukinitenda hivi, nakuomba uniulie mbali, kwamba nimepata fadhili mbele ya macho yako; nami nisiyaone haya mashaka yangu.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 81 :11-16 (K) 1

(K) Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha.

Watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,
Wala Israeli hawakunitaka.
Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,
Waenende katika mashauri yao. (K)

Laiti watu wangu wangenisikiliza,
Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Ningewadhili adui zao kwa upesi,
Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu. (K)

Wamchukiao Bwana wangenyenyekea mbele zake,
Bali wakati wao ungedumu milele.
Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano,
Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani. (K)



SHANGILIO
Zab. 119:34

Aleluya, aleluya,
Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, nitaitii kwa moyo wangu wote.
Aleluya.



INJILI
Mt. 14: 13-21

Yesu aliposikia habari ya kuuawa kwa Yohane Mbatizaji, aliondoka huko katika chombo, akaenda mahali pasipo watu, faraghani. Na makutano waliposikia, walimfuata kwa miguu kutoka miiini mwao. Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu. akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.

Hata kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea, wakasema, Mahali hapa ni nyika tupu, na saa imekwisha pita; uwaage makutano, waende zao vijijini, wakajinunulie vyakula. Yesu akawaambia, Hawana haja kwenda zao, wapeni ninyi kula. Wakamwambia, Hatuna kitu hapa ila mikate mitano na samaki wawili. Akasema, Nileteeni hapa.

Akawaagiza makutano wakati katika majani; akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akabariki, akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi, wanafunzi wakawapa makutano. Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate, vikapu kumi na viwili, vimejaa. Nao waliokula walikuwa wanaume wapata elfu tano, bila wanawake na watoto.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo


Copyright © 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MIMI, NAFSI YANGU, MIMI MWENYEWE!




“MBEGU ZA UZIMA”
Jumapili, Agosti 3, 2025
Dominika ya 18 ya Mwaka C

Mh 1: 2, 2:21-23; 
Zab 90: 3-6, 12-14, 17;
Kol 3: 1-5, 9-11; 
Lk 12: 13-21


MIMI, NAFSI YANGU, MIMI MWENYEWE!


Yesu anafuatwa na mmoja aliyekuwa katika makutano na anamtaka Yesu awe muamuzi kati yake na ndugu yake kuhusu ugawaji wa urithi wao. Yesu, lakini, alikataa kuingilia na kuwa muamuzi wa mambo yao lakini pia anatumia hali ile ili kuwafundisha wafuasi wake, juu ya tamaa ya kujilimbikizia na utajiri. Anawaambia, “angalieni na jihadharini na choyo”, kwakuwa uzima/ maisha ya mtu hayalindwi kwa wingi wa vitu alivyo navyo, na hata angekuwa na vingi kiasi ghani aisivyohitaji. Na hapo anaendelea kuelezea kuhusu mfano wa tajiri mmoja. Itambulike kwamba, huyu tajiri hajaoneshwa kama muovu, wala hajapata mali yake kwa njia zisizo halali au kwa kuwanyonya wengine. Haielezwi katika hali hiyo. Hakika, anaonekana kushangazwa na wingi wa mavuno yake na anafanya jambo ambalo linafikirika ili kuvuna mavuno ya shamba lake. Je, kosa lipo wapi? Tunaweza kujiuliza, kuna kosa ghani, kuhusu kujenga ghala kubwa ili kuhifadhi mavuno yake kwaajili ya baadaye?

Hamna, tunaweza kujibu, isipokuwa vitu viwili. Chakwanza, maswali aliokuwa anajiuliza yeye mwenyewe “Nifanyeje? Maana sina mahali pakuweka akiba mavuno yangu?” na pia alisema, “nitafanya hivi: nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi na hapo nitahifadhi mavuno na vitu vyangu vyote. Na nitaiambia nafsi yangu…..”. Anaisumbukia nafsi yake tu. Hana mawazo yakutaka kushughulika na kusaidia wengine, hakuna alama ya shukrani kwa Baraka alizo pata, hakuna utambuzi wa Mungu kabisa. Bwana shamba huyu tajiri ameangukia katika kuabudu kimungu ambacho ni maarufu sana: “utatu usio mtakatifu wa nafsi, wa, Mimi, mimi binafsi na mimi mwenyewe. Na la pili, anatabiri kuhusu wakati ujao, kwa hili ni mjinga si kwasababu anaongelea kuhusu wakati ujao bali ni kwasababu anadhani anawaze kutegemeza wakati ujao kwa mali yake. 

Pamoja na ukuwaji wa teknologia wa millennia, pamoja na ukuwaji wa maarifa na akili au ukuwaji wa utamaduni, kila mwanadamu na ubinadamu bado unabaki kuwa dhaifu, tegemezi nakuweza kuharibika. Maisha ya mwanadamu katika hali hii yanasumbuliwa na, kutokuwa na uhakika, kukosa ulinzi napengine kwasababu hii tunakazana kujitafutia ulinzi na kujikinga dhidi dharoba za maisha kwa kupitia nguvu na kazi zetu.  

Je, tunapigana vipi na vishawishi vya kutaka kushikilia, kulinda na kujilimbikizia mali ya ulimwengu huu? Kwanza, ukiwa umepewa zaidi, kuwa mtu wa kutoa kwa wengine pia. Kwakutoa kunaleta furaha ambayo utajiri hauwezi kununua. Paulo anatuambia tutenge fedha kila wakati tuweze kutoa kama Bwana anavyotujalia (1 Kor 16: 1-2). Tambua kwamba ni vitu vichache vya milele na jiwekee hazina katika hilo. Jiulize mwenyewe “Nini ninachotaka kuchukua niende nacho wakati nitakapo kufa?”. Vitu ambavyo tunaweza kwenda navyo Mbinguni ni ushuhuda wa watu ambao tuligusa maisha yao kwa njia ya Injili. Hazina ya Kimungu. Kama tutapanga maisha yetu katika vitu vya umilele, hapo tutakuwa tunafanya sahihi kuhusu maisha ya wakati ujao. Na tatu, kama una vingi au vichache, vishikilie katika hali ya wepesi. Usiweke matumaini yako yote katika vitu, vinaweza vikaondoka vyote kutoka katika mikono yako. Mshikilie Mungu daima. Hataondoka ndani mwako milele. 

Sala: Bwana, ponya ugonjwa wa “Mimi mwenyewe” ndani mwangu. Amina

Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, AGOSTI 3, 2025




MASOMO YA MISA, AGOSTI 3, 2025
DOMINIKA YA 18 YA MWAKA C


SOMO 1
Mh. 1:2; 1:21 – 23

Mhubiri asema, Ubatili mtupu ubatili mtupu, mambo yote ni ubatili. Maana kuna mtu ambaye kazi yake ni kwa hekima, na kwa maarifa, na kwa ustadi; naye atamwachia mtu asiyeshughulika nayo kuwa sehemu yake. Hayo tena ni ubatili, nayo ni baa kuu. Kwa maana mtu hupata nini kwa kazi yake yote, na kwa juhudi ya moyo wake alivyojitahidi chini ya jua? Kwa kuwa siku zake zote ni masikitiko, na kazi yake ni huzuni; naam, hata usiku moyoni mwake hamna raha. Hayo ni ubatili.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 94:1 – 2, 6 – 9 (K) 7 – 8

(K) Ingekuwa heri leo msikie sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu.

Njoni tumwimbie Bwana, 
Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
Tuje mbele zake kwa shukrani,
Tumfanyie shangwe kwa zaburi. (K)

Njoni tuabudu tusujudu,
Tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba.
Kwa maana ndiye Mungu wetu,
Na sisi tu watu wa malisho yake,
Na kondoo za mkono wake. (K)

Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
Msifanye migumu mioyo yenu;
Kama vile huko Meriba,
Kama siku ya Masa jangwani.
Hapo waliponijaribu baba zenu,
Wakanipima, wakayaona matendo yangu. (K)



SOMO 2
Kol. 3:1 – 5, 9 – 11

Mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu. Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi. Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika mungu. Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu.

Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu. Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba. Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



SHANGILIO
Efe. 1:17, 18

Aleluya, aleluya!
Ewe Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, uijalie nuru macho ya mioyo yetu, ili tujue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo.
Aleluya.



INJILI
Lk. 12:13 – 21

Mtu mmoja katika mkutano alimwambia, Mwalimu, mwambie ndugu yangu anigawie urithi wetu. Akamwambia, Mtu wewe, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu? Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyonavyo. Akawaambia mithali akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limeza sana; akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule , unywe, ufurahi. Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani? Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.



Copyright © 2025 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

2nd AUGUST 2025


 

CHUKI NA KISASI




ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumamosi, Agosti 2, 2025
Juma la 17 la Mwaka wa Kanisa

Wal. 25:1,8-17
Zab 67:2-3,5-8
Mt. 14:1-12


CHUKI NA KISASI


Katika somo la Injili la leo tunasikia kuhusu kukatwa kichwa kwa Yohane Mbatizaji kwasababu ya ombi la Salome, binti wa Herodia. Yohane alikuwa gerezani kwasababu ya kuongea ukweli kuhusu Herodi kumchukua mke wa nduguye, na hivyo Yohane alichukiwa na Herodia. Hivyo mtoto wa Herodia alivyo cheza vizuri mbele ya Herodi Mfalme na wageni wake, Herodi alipendezwa sana na kucheza kwa binti huyu na hivyo kumwambia aombe lolote kwake naye binti anaomba kichwa cha Yohane mbatizaji baada ya kuomba ushauri kwa mama yake. Hivyo kwanini Herodia na mtoto wake wanaomba kichwa cha Yohane Mbatizaji?

Herodi alikuwa mtu wa kidunia. Pengine Herodia alikuwa na vinywaji vingi sana siku hiyo katika siku hii yake ya kuzaliwa; na katika furaha hii anafanya uamuzi ambao sio wa hekima, ambao Herodia anatumia muda huu kutimiza maovu yake. Herodi anafanya uamuzi ambao yeye mwenyewe hakutaka hivyo anaogopa kutenda mema. Anajazwa na chuki ya mke wake huyu na hivyo, anaamua Yohane akatwe kichwa yeye ambaye alikuwa amemzoea kumsikiliza na kufurahi. Herodia hakuwa na dhamiri hai yenye kumkataza kufanya uovu. Aina hii ya chuki inaeleza jinsi ghani chuki ilivyo mbaya inavyokuwa kubwa huleta madhara. Wakati hasira inavyokuwa huleta madhara makubwa mno na kusababisha uharabifu mkuwa sana katika maisha yetu na ya watu. Hali hii ya hasira inapaswa kufanyiwa toba na kusamehewa mwanzoni kabisa kabla haijawa kubwa.

Tafakari leo, je, umeshikilia hasira ambayo ni mbaya na kinyongo moyoni mwako katika hali yeyote? Je, hasira hiyo inakuwa nakusababisha hasara kwako na kwa wengine? Kama ndiyo hivyo, jitahidi kuiacha na samehe na anza maisha mapya. Ndilo jambo jema ambalo waweza kulifanya.

Sala: Bwana, ni pe neema ninayo hitaji ili niweze kutazama moyo wangu au uchungu wowote ndani yangu au chuki yeyote ile. Nisafishe Bwana na nakuomba unifanye niwe huru. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2019 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com


MASOMO YA MISA, AGOSTI 2, 2025




MASOMO YA MISA, AGOSTI 2, 2025
JUMAMOSI, JUMA LA 17 LA MWAKA


SOMO 1
Wal. 25:1,8-17

Bwana alinena na Musa katika mlima wa Sinai, na kumwambia: Utajihesabia sabato za miaka, maana, miaka saba mara saba; zitakuwa ni siku za sabato saba za miaka kwenu, maana miaka arobaini na kenda. Ndipo utakapoipeleka pande zote hiyo baragumu yenye sauti kuu, siku ya kumi ya mwezi wa saba; katika siku hiyo ya upatanisho mtaipeleka baragumu katika nchi yenu yote. Na mwaka wa hamsini mtautakasa, na kupiga mbiu ya kuachwa mahuru katika nchi yote kwa watu wote waiketio; itakuwa ni yubile kwenu; nanyi kila mtu atairudia milki yake mwenyewe, nanyi mtarejea kila mtu kwa jamaa yake. Mwaka huo wa hamsini utakuwa ni yubile kwenu; msipande mbegu, wala msivune kitu hicho kimeacho chenyewe, wala msizitunde zabihu za mizabibu isiyopelewa. Kwa kuwa ni yubile; utakuwa mwaka mtakatifu kwenu; mtakula maongeo yake yatokayo shambani.

Mwaka huo wa yubile mtairudia kila mtu milki yake. Tena kama ukimwuzia jirani yako chochote, au kununua chochote mkononi mwa jirani yako, msidanganyane wenyewe kwa wenyewe; kwa hesabu ya miaka iliyo baada ya yubile ndivyo utakavyonunua kwa jirani yako, na kama hesabu ya miaka ya mavuno ndivyo atakavyokuuzia wewe. Kama hesabu ya miaka ilivyo ni nyingi ndivyo utakavyoongeza bei yake, na kama hesabu ya miaka ilivyo ni chache ndivyo utakavyopunguza bei yake; kwani yeye akuuzia mavuno kama hesabu yake ilivyo. Wala msidanganyane; lakini utamcha Mungu wako; kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 67:1-2, 4- 6-7 (K) 3

(K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru.

Mungu na atufadhili na kutubariki,
Na kutuangazia uso wake.
Njia yake ijulikane duniani,
Wokovu wake katikati ya mataifa yote. (K)

Mataifa na washangilie,
Naam, waimbe kwa furaha,
Maana kwa haki utawahukumu watu,
Na kuwaongoza mataifa walioko duniani. (K)

Nchi imetoa mazao yake;
Mungu, Mungu wetu, ametubariki.
Mungu atatubariki sisi;
Miisho yote ya dunia itamcha Yeye. (K)



SHANGILIO
Zab. 25:4,5

Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, unijulishe njia zako, unifundishe mapito yako.
Aleluya.



INJILI
Mt. 14:1 – 12

Mfalme Herode alisikia habari za Yesu, akawaambia watumishi wake, Huyo ndiye Yohane Mbatizaji; amefufuka katika wafu; na kwa hiyo nguvu hizo zinatenda kazi ndani yake.

Maana Herode alikuwa amemkamata Yohane, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye. Kwa sababu Yohane alimwambia, Si halali kwako kuwa naye. Naye alipotaka kumwua, aliwaogopa watu, maana walimwona Yohane kuwa nabii. Hata ilipofika sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti Herodia alicheza mbele ya watu, akampendeza Heorode. Hata akaahidi kwa kiapo ya kwamba atampa lolote atakaloliomba. Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohane Mbatizaji.

Naye mfalme akasikitika; lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya wale walioketi chakulani pamoja naye, akaamuru apewe; akatuma mtu akamkata kichwa Yohane mle gerezani. Kichwa chake kikaletwa katika kombe, akapewa yule kijana; akakichukua kwa mamaye. Wanafunzi wake wakaenda, wakamchukua yule maiti, wakamzika; kisha wakaenda wakampasha Yesu habari.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Copyright © 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

UDONGO WENYE RUTUBA WENYE KUPOKEA BARAKA ZA MUNGU



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Ijumaa Agosti 1, 2025
Juma la 17 la Mwaka

Kumbukumbu ya Mtakatifu Alfonsi Maria wa Liguori

Wal. 23:1,4-11,15-16,27,34-37
Zab 8:2-5, 9-10 (k) 1,
Mt. 13:54-54


UDONGO WENYE RUTUBA WENYE KUPOKEA BARAKA ZA MUNGU

Yesu alitembelea katika mji wake mwenyewe Nazareth lakini anashangaa watu hawapo tayari kumkaribisha na kupokea ujumbe wa habari njema. Hawakatai tu kumwamini na ujumbe wake na miujiza yake, wanamhukumu kwa kutazama historia ya maisha yake ya kifamilia. “huyu si mwana wa seremala?” Mama yake sio Mariam? Walimtazama yeye kama mtu wa kawaida tu. Na hivyo wanazuia ufalme wa Mungu unaokuja katikati yao.

Sehemu hii inatufundisha sisi kwamba tuwe tayari kuwasikiliza wenzetu, hasa wale waliojifunza na wenye hekima hata kama ni ndugu zetu. Kwani Mungu anaweza kutufundisha sisi hata kwa kutumia ndugu zetu wa familia. Pili tunapaswa kujirekebisha hasa tunapo amua kumhukumu mtu kwa kutumia familia yake au historia yake. Watu wote hawabaki walivyo kama zamani. Tunapaswa kuwatazama watu katika hali ya mtazamo mpya na sio kumfungia katika kisanduku kwamba hatabadilika. Tatu, mara nyingi tunasikia mandiko matakatifu kupitia kwa watu mbali mbali, tunapaswa kusikiliza sauti ya Roho Mtakatifu anaye ongea nasi kwa njia ya mtu huyo. Nne, usikatishwe tamaa na mtu aliyekuchukia kwasababu ya hali ya familia yako au ahali yako ya zamani, au kwasababu hakupendi. Zaidi ya yote usiache kutenda mema kwa watu wote.

Mabadiliko ya kweli kwa roho za watu wa Nazaret hazikubadilika kwasababu ya kukosa Imani. Watu hawakuwa tayari kupokea maneno ya Yesu yazame katika mioyo yao na akili zao. Kwa njia hiyo, Yesu, hakuweza kufanya miujiza mikuu huko katika mji wake wenyewe.

Je, unamruhusu Yesu abadilishe kila kitu katika maisha yako ya kila siku? Je, upo tayari kumfanya afanye miujiza mikubwa katika maisha yako? Kama una wasi wasi katika kujibu maswali haya ni dalili kwamba unamhitaji Mungu afanye mabadiliko katika maisha yako.

Sala: Bwana, ninaomba roho yangu iweze kuwa udongo mzuri wa kuotesha neno lako. Ninaomba roho yangu iweze kubadilishwa nawe, paweze kuwa sehemu ya neno lako na uwepo wako. Ninaomba unibadilishe mimi na kunifanya niweze kuwa chombo cha Amani ya neema yako. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, IJUMAA, AGOSTI 1, 2025



MASOMO YA MISA, IJUMAA, AGOSTI 1, 2025
JUMA LA 17 LA MWAKA 

Kumbukumbu ya Mtakatifu Alfonsi Maria wa Liguori


SOMO 1
Law. 23 :1, 4-11,15-16,27, 34-37

Bwana alinena na Musa, na kumwambia: Sikukuu za Bwana ni hizi, ni makusanviko matakatifu, ambayo mtayapigia mbiu kwa nyakati zake. Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi wakati wa jioni, ni pasaka ya Bwana. Na siku ya kumi na tano ya mwezi ule ule ni sikukuu kwa Bwana ya mkate usiotiwa chachu; mtaila mikate isiyochachwa muda wa siku saba.

Siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi. Lakini mtasongeza sadaka kwa Bwana kwa njia ya moto siku saba; siku ya saba ni kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi.

Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Hapo mtakapokuwa mmekwisha ingia hiyo nchi niwapayo, na kuyavuna mavuno yake, ndipo mtakapomletea kuhani mganda wa malimbuko ya mavuno yenu; naye atautikisa mganda mbele za Bwana ili kwamba ukubaliwe kwa ajili yenu; siku ya pili baada ya sabato kuhani atautikisa.

Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia sabato saba; hata siku ya pili ya hiyo sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya unga mpya.

Lakini siku ya kumi ya mwezi huo wa saba ni siku ya upatanisho; itakuwa kusanyiko takatifu kwenu, nanyi mtazitesa nafsi zenu; nanyi mtaso- ngeza sadaka kwa Bwana kwa njia ya moto. Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba ni sikukuu ya vibanda muda wa siku saba kwa Bwana.

Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi. Mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto siku saba; siku ya nane kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto; ni mkutano wa makini huu; msifanye kazi yo yote ya utumishi.

Sikukuu za Bwana ni hizi, ambazo mtazipigia mbiu ya kuwa ni makusanyiko matakatifu, ili mmsongezee Bwana sadaka kwa moto, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya unga, na dhabihu, na sadaka za kinywaji, kila sadaka kwa siku yake.

Neno la Mungu...Tumshukuru Mungu


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 8: 2-5, 9-10 (K) 1

(K) Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha.

Pazeni zaburi, pigeni matari,
Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
Pigeni panda mwandamo wa mwezi,
Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu. (K)

Kwa maana ni sheria kwa Israeli,
Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.
Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu,
Alipoondoka juu ya nchi ya Misri;
Maneno yake nisiycmjua naliyasikia. (K)

Usiwe na mungu mgeni ndani yako;
Wala usimsujudie mungu mwingine.
Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,
Niliyekupandisha toka nchi ya Misri;
Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza. (K)


SHANGILIO
1 The 2: 13

Aleluya, aleluya, Lipokeeni neno la Mungu, siyo kama neno la wanadamu, bali kama neno la Mungu. Aleluya.


INJILI
Mt. 13: 54-58

Yesu alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? Huyu si mwana wa seremala? mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda? Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote? Wakachukizwa nave. Yesu akawaambia, Nabii ha- kosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe. Wala hakufanya miujiza mingi huko, kwa sababu ya kutokuamini kwao.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo



Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.