Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu
KUOMBA HURUMA
ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Alhamisi, Septemba 18, 2025,
Juma la 24 la Mwaka
1Tim 4:12-16
Zab. 111:7-10
Lk7: 36-50.
KUOMBA HURUMA
Somo la Injili linatuambia kuhusu Farisayo mmoja aliye mwalika Yesu kwa mlo. Baada ya Yesu kuingi katika nyumba ya Farisayo anakuja mama mmoja mwenye dhambi na kuja na mafuta na kumpaka miguuni huku akilia na kupangusa miguu ya Yesu kwa nyewele zake na kuibusu miguu yake na kuipaka mafuta. Mafarisayo wanatoa hukumu kwa huyu Mama pamoja na Yesu. Yesu anamrekebisha kama alivyofanya kwa Mafarisyo wengi.
Mama huyu anaonesha mapendo kwa Yesu na moyo uliojaa huzuni kuhusu dhambi na kuwa na unyenyekevu. Dhambi yake ilikuwa kubwa na kwa matokeo yake lakini pia unyenyekevu wake na upendo wake ulikuwa mkubwa pia. Unaonekana katika matendo yake kama alivyokuja kwa Yesu.
Kwanza, “alisimama nyuma ya Yesu…”
Pili, alianguka chini miguuni pa Yesu…”
Tatu, alikuwa akilia…”
Aliosha miguu yake kwa machozi yake…”
Tano, alikausha miguu ya Yesu kwa nywele zake…”
Sita, alibusu miguu yake.
Saba, aliipaka miguu yake mafuta ya bei ya juu.
Kama tukio hili sio tukio la majuto makuu, toba na unyenyekevu basi itakuwa ni vigumu kujaribu kuelewa nikitu gani tofauti. Ni unyoofu wa hali ya juu na kwa njia hii aligusa huruma ya Yesu bila hata kusema neno lolote.
Tafakari leo juu ya dhambi zako mwenyewe. Usipo itambua dhambi yako huwezi kuwa na unyenyekevu na toba hii ya namna hii. Je, unatambua dhambi yako? Kuanzia pale anza kufikiria jinsi ya kuanguka magotini pa Yesu nakuomba huruma yake. Jitahidi kulifanya hilo na Yesu atakufanyia yale yale aliomfanyia yule mwananmke.
Sala: Bwana, ninaomba huruma yako. Mimi ni mdhambi na nastahili adhabu. Ninakiri dhambi zangu. Ninakuomba unisamehe dhambi zangu na unipe huruma yako juu yangu. Yesu nakuamini wewe. Amina
Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
MASOMO YA MISA, ALHAMISI, SEPTEMBA 18, 2025
MASOMO
YA MISA,
ALHAMISI, SEPTEMBA 18, 2025
JUMA
LA 24 LA MWAKA
________
SOMO
1
1Tim 4:12-16
Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi. Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha. Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee. Uyatafakari hayo; ukae katika hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote. Jitunze nafsi yako, na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia.
________
WIMBO
WA KATIKATI
Zab. 111:7-10
(K) Matendo ya Bwana ni makuu.
Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu,
Maagizo yake yote ni amini,
Yamethibitika milele na milele,
Yamefanywa katika kweli na adili. (K)
Amewapelekea watu wake ukombozi,
Ameamuru agano lake liwe la milele,
Jina lake ni takatifu la kuogopwa. (K)
Kumcha Bwana ndio mwanzo wa hekima,
Wote wafanyao hayo wana akili njema,
Sifa zake zakaa milele. (K)
________
SHAGILIO
1Pet.
1:25
Aleluya,
aleluya,
Neno
la Bwana hudumu hata milele, na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa
kwenu.
Aleluya.
________
INJILI
Lk 7:36-50
Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani. Na tazama, mwanamke mmoja wa mji ule, aliyekuwa mwenye dhambi, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu. Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.
Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi. Yesu akajibu akamwambia, Simoni, nina neno nitakalo kukuambia. Akasema, Mwalimu, nena. Akasema, Mtu mmoja mkopeshaji alikuwa na wadeni wawili; mmoja amwia dinari mia tano, na wa pili hamsini. Nao walipokuwa hawana cha kumlipa, aliwasamehe wote wawili. Katika hao wawili ni yupi atakayempenda zaidi? Simoni akajibu akasema, Nadhani ni yule ambaye alimsamehe nyingi. Akamwambia, Umeamua haki.
Akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, Wamwona mwanamke huyu? Niliingia nyumbani kwako, hukunipa maji kwa miguu yangu; bali huyu amenidondoshea machozi miguu yangu, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake. Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu. Hukunipaka kichwa changu mafuta; bali huyu amenipaka miguu yangu marhamu. Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo. Kisha alimwambia mwanamke, Umesamehewa dhambi zako. Ndipo wale walioketi chakulani pamoja naye walianza kusema mioyoni mwao, Ni nani huyu hata asamehe dhambi? Akamwambia yule mwanamke, Imani yako imekuokoa, enenda zako kwa amani.
Neno
la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Copyright
© 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora
– Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
KUFUNGUA MIOYO YETU KWA YESU
“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Septemba 17, 2025
Juma la 24 la Mwaka
Jumatano, Septemba 17, 2025
Juma la 24 la Mwaka
1 Kor 12:31 – 13:13;
Zab 32: 2-5, 12, 22;
Lk 7: 31-35.
KUFUNGUA MIOYO YETU KWA YESU
Kwenye somo la injili Yesu anakishangaa kizazi hiki kwani kinachezewa ngoma, kinaambiwa kifanye jambo hili lakini basi hakifuati. Kina ukaidi mkubwa na ukosefu wa upendo na hivyo basi kimeshindwa kutambua na kusoma alama za ulimwengu. Hii yote ni kwa sababu kilikosa upendo na kuwa na majivuno. Kikaona watu kama akina Yohane Mbatizaji na Yesu kama vituko tu. Kilitaka mawazo na mipango yao ifuate hali ya kuachana na wengine.
Sisi tuachane na mawazo kama haya ya hiki kizazi kwa kuwa watu wenye upendo zaidi, mshikamano na kuacha majivuno. Majivuno yametufanya tusiwe wa faida ndani ya ulimwengu.
MASOMO YA MISA, JUMATANO, SEPTEMBA 17, 2025
MASOMO YA MISA, JUMATANO, SEPTEMBA 17, 2025
JUMA LA 24 LA MWAKA
________
________
SOMO I
1 Tim 3: 14-16
Nakuandikia hayo, nikitaraji kuja kwako hivi karibu. Lakini nikikawia, upate kujua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli. Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu:
Mungu alidhihirishwa katika mwili,
Akajulika kuwa na haki katika roho,
Akaonekana na malaika,
Akahubiriwa katika mataifa,
Akaaminiwa katika ulimwengu,
Akachukuliwa juu katika utukufu.
Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 111: 1-6
(K.) Matendo ya Bwana ni makuu. Au: Aleluya.
Nitamshukuru Bwana kwa moyo wangu wote,
Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano.
Matendo ya Bwana ni makuu.
Yafikiriwa sana na wapendezwao nayo. (K.)
Kazi yake ni heshima na adhama,
Na haki yake yakaa milele.
Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu;
Bwana ni mwenye fadhili na rehema. (K.)
Amewapa wamchao chakula;
Atalikumbuka agano lake milele.
Amewajulisha watu wake uwezo wa matendo yake,
Kwa kuwapa urithi wa mataifa. (K.)
________
Lk 6: 63,68
Aleluya, aleluya,
Maneno yako, Bwana, ni roho na uzima.
Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
Aleluya.
________
INJILI
Lk. 7:31-35
Wakati ule: Jesu aliwaambia makutano, "Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki, nao wamefanana na nini? Wamefanana na watoto walioketi sokoni na kuitana, wakisema, 'Tuliwapigia filimbi wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.'
Kwa kuwa Johane Mbatizaji alikuja, hali mkate wala hanywi divai, nanyi mwasema, 'Ana pepo.' Mwana wa Adamu amekuja, anakula na kunywa, nanyi mwasema, 'Tazama, mlafi huyu, na mnywaji wa divai, rafiki wao watoza ushuru na wenye dhambi.' Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote."
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________
Copyright © 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
TUTENDE KWA HURUMA!
“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumanne, Septemba 16, 2025,
Juma la 24 la Mwaka
1 Tim 3:1-13
Zab 101: 1-3, 5-6
Lk 7: 11-17.
TUTENDE KWA HURUMA!
Injili ya leo inatupa simulizi la kumfufua mtoto wa Mjane wa Naimu. Kwa maneno machache Luka anafanikiwa kutoa taswira nzuri ya jinsi pande zote mbili walivyokutana. Upande wa waliobeba mtoto aliyekufa (wafu) wa mjane wanaotoka njee ya mji kuelekea makaburini na upande wa Yesu (uzima) na umati unaomfuata wanaoingia mjini. Ni huruma iliomsukuma Yesu katika kusema na kutenda. Huruma hapa inaweza kutafsiriwa kama “kuteseka na” kujihisi au kufanya mateso ya mwenzako ni yako, kujitambua mwenyewe pamoja na mwenzako, kuhisi uchungu na mateso ya mwenzako. Ni huruma iliofanya nguvu ya Yesu iweze kutenda, nguvu ya uwezo wake juu ya kifo. Je, mateso, uchungu wa wengine unagusa roho yangu na kuwa na huruma? Je mimi nina saidia wengine waweze kuondokana na machungu yao na kujenga maisha mapya?
Sala: Bwana niinue tena, wakati nikiwa sina nguvu na nikiwa na mashaka. Amina
Zab 101: 1-3, 5-6
Lk 7: 11-17.
TUTENDE KWA HURUMA!
Injili ya leo inatupa simulizi la kumfufua mtoto wa Mjane wa Naimu. Kwa maneno machache Luka anafanikiwa kutoa taswira nzuri ya jinsi pande zote mbili walivyokutana. Upande wa waliobeba mtoto aliyekufa (wafu) wa mjane wanaotoka njee ya mji kuelekea makaburini na upande wa Yesu (uzima) na umati unaomfuata wanaoingia mjini. Ni huruma iliomsukuma Yesu katika kusema na kutenda. Huruma hapa inaweza kutafsiriwa kama “kuteseka na” kujihisi au kufanya mateso ya mwenzako ni yako, kujitambua mwenyewe pamoja na mwenzako, kuhisi uchungu na mateso ya mwenzako. Ni huruma iliofanya nguvu ya Yesu iweze kutenda, nguvu ya uwezo wake juu ya kifo. Je, mateso, uchungu wa wengine unagusa roho yangu na kuwa na huruma? Je mimi nina saidia wengine waweze kuondokana na machungu yao na kujenga maisha mapya?
Sala: Bwana niinue tena, wakati nikiwa sina nguvu na nikiwa na mashaka. Amina
MASOMO YA MISA, JUMANNE, SEPTEMBA 16, 2025
MASOMO YA MISA, JUMANNE, SEPTEMBA 16, 2025
JUMA LA 24 LA MWAKA
________
SOMO I
1 Tim 3: 1-13
Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?) Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu. wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia. Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote. Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao. Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu.
Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 100: 1-3, 5-6
(K.) Nitakwenda kwa unyofu wa moyo
Rehema na hukumu nitaziimba,
Ee Bwana, nitakuimbia zaburi.
Nitaiangalia njia ya unyofu;
Utakuja kwangu lini? (K.)
Nitakwenda kwa unyofu wa moyo
Ndani ya nyumba yangu.
Sitaweka mbele ya macho yangu
Neno la uovu. (K.)
Amsingiziaye jirani yake kwa siri,
Huyo nitamharibu.
Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno,
Huyo sitavumilia naye. (K.)
Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,
Hao wakae nami.
Yeye aendaye katika njia kamilifu,
Ndiye atakayenitumikia. (K.)
________
Lk 7:16
Aleluya, aleluya,
Nabii mkuu ametokea kwetu;
na Mungu amewaangalia watu wake.
Aleluya.
________
INJILI
Lk. 7:11-17
Yesu alikwenda mpaka mji mmoja uitwao Naini, na wanafunzi wake walifuatana naye pamoja na mkutano mkubwa. Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye. Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie. Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka. Yule maiti akainuka, akaketi, akaanza kusema. Akampa mama yake. Hofu ikawashika wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Nabii mkuu ametokea kwetu; na, Mungu amewaangalia watu wake. Habari hii yake ikaenea katika Uyahudi wote, na katika nchi zote za kando kando.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________
Copyright © 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
KUTESEKA KWA AMANI NA FURAHA!
“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatatu, Septemba 15, 2025
Juma la 24 la Mwaka wa Kanisa
Kumbukumbu ya Bikira Maria Mtakatifu wa Mateso
Ebr 5: 7-9; au 1Kor 15:1-11
Zab 30: 2-6, 15-16, 20;
Yn 19: 25-27, 35 au Lk 2: 33-35
KUTESEKA KWA AMANI NA FURAHA!
Leo tunakumbuka mateso ya Mama yetu Bikira Maria. Mateso ya Maria yalikuwa
ya ndani. Bikira Maria alikuwa mwanadamu kamili kwasababu hakutenda dhambi na
kati ya watu waliompendeza Mungu katika hali ya ukamilifu wote ni Bikira Maria
licha ya Mwanae, lakini kwa ajili ya hili hatuwezi kusema hakuwa na hisia ya
kuhisi mambo ya duniani. Kwasababu ya ukamilifu wake, alipenda kwa mapendo ya
ndani kuliko sisi. Kwasababu ya upendo huu, alihisi uchungu wa kumpoteza mwanae
kuliko sisi. Mateso ya Maria tofauti na yetu yalikuwa kamili. Mateso yetu mara
nyingi yamechanganyika na udhaifu wetu. Maria hakuhuzunika kwasababu atamkosa
Mwanae ampe msaada. Aliteseka kwasababu aliona mateso ya yule anaye mpenda, na
akahisi mateso yale kama Mwanae alivyohisi. Tunaweza kuhisi pia ni kwa jinsi
ghani Yesu alivyojisikia alivyomuona Mamaye katika huzuni. Ni hakika
ilimsababishia mateso pia, lakini ilikuwa pia ni hali ya kuonesha ukaribu wao.
Ulimwengu mzima unaweza kuwa umekuwa wa ukatili na hali zote, lakini uso wa
Mama yake ulikuwa ni sehemu pekee alioweza kuelekezea macho yake, akiona sura
na mfano aliouweka wakati anatuumba sisi.
Huzuni ya mama haikuwa ni huzuni bila matumaini. Alijua kwa matumani fulani
kwamba Mwanae atafufuka kutoka wafu. Tumaini lake halikumzuia kuhisi uchungu na
wala halikumzuia kutazamia ufufuko wake. Maria ni Mama yetu. Kama ilivyo kwa
Mama mwema, anatufundisha sisi. Tunapaswa tutuoe muda wetu tukiwa naye katika
mti wa Msalaba, tukimuomba atufundishe jinsi ya kuhisi nasi mateso yetu katika
maisha. Tusisite kumkimbilia atuombee tunapokumbana na adha na mateso katika
maisha, yeye awe faraja na msaada wetu kwani atakuwa nasi, akisimama nasi na
kuteseka nasi, akiyaweka yote chini ya Msalaba wa Mwanae kwa niaba yetu.
Sala: Mama wa Upendo, Mama wa Mateso na Mama wa huruma, utuombee sisi.
Amina
Subscribe to:
Posts (Atom)