Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

NOVENA YA NOELI - SIKU YA PILI - 17 Desemba 2025



W: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu.

W: Furahi, ee binti Sion, na shangilia sana, ee binti Yerusalem! sikia, Bwana atafika na siku ile utatokea mwanga mkuu, na milima itatonesha utamu; na vi-lima vitatiririsha maziwa na asali, kwa sababu atafika nabii mkuu, na Yeye atageuza Yerusalem.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu.

W: Sasa Mungu-Mtu wa nyumba ya Daudi atakuja kuketi juu ya kiti cha enzi, mtamwona na moyo wenu utafurahi.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

W: Sikia, atafika Bwana na Mlinzi wetu, Mtakatifu wa Israel. Kichwani mwake ana taji la ufalme wake: atatawala nchi toka bahari mpaka bahari, toka mto mpaka ukingoni mwa dunia.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

Sikia, Bwana ataonekana, hadanganyi hata: akikawia mngoje, kwani atafika tu, hawezi kuchelewa.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

Bwana atashuka kama mvua juu ya ngozi yenye manyoya: katika siku zake kutakuwa na haki na amani tele; na wafalme wote wa dunia watamwa-budu, na makabila yote yatamtumikia.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

Mtoto atazaliwa kwa ajili yetu na ataitwa Mungu mwenye nguvu: atakalia kiti cha ezi cha Daudi baba yake; atatawala, na begani atachukua firhbo ya uwezo wake.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

Ee Bethlehem, mji wa Mungu mkuu, kwako atatokea Mtawala wa Israel: na uzazi wake ni wa milele, atatukuzwa katika dunia yote; na atakapofika ita-kuwa amani humu duniani mwetu.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

ZABURI
Mbingu ifurahi nayo dunia ishangilie,
nanyi mi-lima pigeni vigelegele.

Milima ionyeshe furaha,
na vilima vitoe haki.

Sababu Bwana wetu atafika,
na atawahurumia maskini wake.

Ee mbingu, nyesheni umande
na mawingu yatuletee

Mtakatifu, nchi ifunguke
na imzae mkombozi.

Utukumbuke, ee Bwana,
na utuletee wokovu wako.

Ee Bwana, utuonyeshe huruma yako,
nautupe ukombozi wako.

Ee Bwana, umlete Mwana - Kondoo mfalme wa dunia; atakayetawala toka jiwe la jangwani mpaka mlima wa binti Sion.

Njoo utukomboe, ee Bwana, Mungu wa Majeshi:
utuonyeshe uso wako na tutaokoka.

Njoo, ee Bwana, utuletee amani yako:
ili tufurahi mbele yako kwa moyo safi.

Tupate kujua njia yako humu duniani, ee Bwana:
na tujue wokovu wako katika makabila yote.

Ee Bwana, amsha nguvu zako na ufike:
ili utukomboe.

Njoo, ee Bwana, usikawie:
uliondolee taifa lako dhambi.

Ee, laiti ungepasua mbingu na kushuka:
milima ingeyeyuka mbele yako.

Njoo, ee Bwana, utuonyeshe uso wako:
wewe unayeketi juu ya Malaika.

Atukuzwe Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu
kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.

WIMBO WA BIKIRA MARIA
K: Ee hekima uliyetoka mdomoni mwa Yule aliye juu, unayeenea toka mwanzo mpaka mwisho, unayeongoza yote kwa nguvu na upole, uje utufundishe njia ya busara.

Moyo wangu wamtukuza Bwana,
Roho yangu inafurahi
kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.

Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma,
mtumishi wake mdogo,
Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu,
jina lake ni takatifu.

Huruma yake kwa watu wanaomcha
hudumu kizazi hata kizazi.

Amefanya mambo makuu kwa mkono wake:
amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;

amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi,
akawakweza wanyenyekevu.

Wenye njaa amewashibisha mema,
matajiri amewaacha waende mikono mitupu.

Amempokea Israeli mtumishi wake,
akikumbuka huruma yake.

Kama alivyowaahidia wazee wetu,
Abrahamu na uzao wake hata milele.

K: Ee hekima uliyetoka mdomoni mwa Yule aliye juu, unayeenea toka mwanzo mpaka mwisho, unayeongoza yote kwa nguvu na upole, uje utufundishe njia ya busara.


Sala: Ee Bwana twakusihi uharikishe wala usichelewe na utuletee nguvu ya juu, kusudi wote wanaotumainia huruma yako wapate kufariji wana majilio yako, unayeishi na kutawala milele. Amina

JE, UNATAMBUA MPANGO WA MUNGU JUU YAKO?



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano, Desemba 17, 2025
Juma la 3 la Majilio

Mwa 49: 2, 8-10;
Zab 71: 1-4, 7-8, 17;
Mt 1: 1-17


JE, UNATAMBUA MPANGO WA MUNGU JUU YAKO?


Leo, tunaingia kwenye ‘oktava’ ya kujiandaa kwa karibu kabisa kwa ujio wa Kristo. Kwa siku hii, tunasikia historia ya ukoo wa Yesu. Matayo anatueleza katika mtiririko wa hali tatu ya vizazi kumi na nne. Anaanza na Abrahamu na kumalizia na Yesu. Injii inaanza kwa kumwita Yesu kuwa ni Mwana wa Daudi, Mwana wa Abraham. Hii inaonyesha muunganiko kutoka tangu ahadi za Mungu kwa Abraham, mpaka utimilifu wake katika nafsi ya Bwana wetu Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

Katika kutimiza ahadi hii, tunaona kwamba Mungu ni mwaminifu. Inachukua karne na karne, ili ahadi yake kwa Abraham itimie, lakini kwa hakika ilitimia. Hili linatueleza wazi kwamba muda wa Mungu na mpango wake juu yetu anajua muda wake wakutimiza ahadi zake, tofauti na jinsi tunavyoweza kufikiri. Tunaweza kuja na mawazo mazuri tukidhani kwamba yatapita. Lakini mara yasipopita mara moja kwa jinsi tunavyodhani na kutumaini, tunaanza kukata tamaa.

Tutafakari juu ya mipango alionayo Mungu juu ya maisha yetu. Inaweza isiwe kama tunavyodhani na kutabiri au kadiri ya jinsi tunavyoomba katika sala. Lakini inaridhisha kwamba ni kwa ajili ya uzuri wetu, ni kwasababu ya muunganiko wetu naye Mbinguni. Yesu alizaliwa ili atuvute karibu zaidi nae. Leo Yesu anatutaka mimi na wewe tuweke mipango yetu kwake na mitazamo yetu kwake. Anahitaji haya na mengine mengi. Anataka tujikabidhi sisi wenyewe kwenye mpango wake mkamilifu ndani ya moyo wa Baba yetu wa Mbinguni.

Sala: Bwana, natambua kwamba njia zako ni kamilifu na kwamba mipango yako ni mikamilifu sio yangu. Nisaidie niachane na tamaa zangu na nijikabidhi zaidi kwako, na kukuamini kabisa, na kwa yote uliopanga kwa ajili yangu. Bwana, hekima yako ni kamilifu. Nisaidie niweze kuamini hilo kwa moyo wangu wote. Yesu nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, DESEMBA 17, 2025

 

MASOMO YA MISA, DESEMBA 17, 2025

Jumatano ya 3 ya Majilio


SOMO 1
Mwa 49:2, 8-10

Yakobo akawaita wanawe akawaambia; Kusanyikeni, msikie, enyi wana wa Yakobo, Msikilizeni Israeli, baba yenu. Yuda, ndugu zako watakusifu, Mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako. Wana wa baba yako watakuinamia. Yuda ni mwana-simba, Kutoka katika mawindo, mwanangu, umepanda; Aliinama akajilaza kama simba, Na kama simba mke; ni nani atakaye mwamsha? Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake, Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki, Ambaye mataifa watamtii.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 72:1-4, 7-8, 17

(K) Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi, na wingi wa amani hata mwezi utakapokoma.

Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako,
Na mwana wa mfalme haki yako.
Atawaamua watu wako kwa haki,
Na watu wako walioonewa kwa hukumu. (K) 

Milima itawazalia watu amani,
Na vilima navyo kwa haki.
Atawahukumu walioonewa wa watu,
Atawaokoa wahitaji, (K) 

Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi,
Na wingi wa amani hata mwezi utakapokoma.
Na awe na enzi toka bahari hata bahari,
Toka Mto hata miisho ya dunia. (K)

Jina lake na lidumu milele,
Pindi ling'aapo jua jina lake liwe na wazao;
Mataifa yote na wajibariki katika yeye, Na kumwita heri. (K) 


SHANGILIO

Aleluya, aleluya,
Ee Hekima ya Aliye juu, unayepanga yote kwa nguvu zako na utaratibu mwema, uje kutufunza njia ya busara.
Aleluya.


INJILI
Mt 1:1-17

Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu. Ibrahimu alimzaa Isaka; Isaka akamzaa Yakobo; Yakobo akamzaa Yuda na ndugu zake; Yuda akamzaa Peresi na Zera kwa Tamari; Peresi akamzaa Esromu; Esromu akamzaa Aramu; Aramu akamzaa Aminadabu; Aminadabu akamzaa Nashoni; Nashoni akamzaa Salmoni; Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu; Boazi akamzaa Obedi kwa Ruthu; Obedi akamzaa Yese; Yese akamzaa mfalme Daudi. Sulemani akamzaa Rehoboamu; Rehoboamu akamzaa Abiya; Abiya akamzaa Asa; Asa akamzaa Yehoshafati; Yehoshafati akamzaa Yoramu; Yoramu akamzaa Uzia; Uzia akamzaa Yothamu; Yothamu akamzaa Ahazi; Ahazi akamzaa Hezekia; Hezekia akamzaa Manase; Manase akamzaa Amoni; Amoni akamzaa Yosia; Yosia akamzaa Yekonia na ndugu zake, wakati wa ule uhamisho wa Babeli. Na baada ya ule uhamisho wa Babeli, Yekonia akamzaa Shealtieli; Shealtieli akamzaa Zerubabeli; Zerubabeli akamzaa Abihudi; Abihudi akamzaa Eliakimu; Eliakimu akamzaa Azori; Azori akamzaa Sadoki; Sadoki akamzaa Akimu; Akimu akamzaa Eliudi; Eliudi akamzaa Eleazari; Eleazari akamzaa Matani; Matani akamzaa Yakobo; Yakobo akamzaa Yusufu mumewe Mariamu aliyemzaa YESU aitwaye Kristo. Basi vizazi vyote tangu Ibrahimu hata Daudi ni vizazi kumi na vinne; na tangu Daudi hata ule uhamisho wa Babeli ni vizazi kumi na vinne; na tangu ule uhamisho wa Babeli hata Kristo ni vizazi kumi na vinne.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

NOVENA YA NOELI - SIKU YA KWANZA - 16 Desemba 2025



NOVENA YA NOELI, SIKU YA KWANZA
16 Desemba 2025

W: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu. 

W: Furahi, ee binti Sion, na shangilia sana, ee binti Yerusalem! sikia, Bwana atafika na siku ile utatokea mwanga mkuu, na milima itatonesha utamu; na vi-lima vitatiririsha maziwa na asali, kwa sababu atafika nabii mkuu, na Yeye atageuza Yerusalem. 
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu. 

W: Sasa Mungu-Mtu wa nyumba ya Daudi atakuja kuketi juu ya kiti cha enzi, mtamwona na moyo wenu utafurahi. 
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

W: Sikia, atafika Bwana na Mlinzi wetu, Mtakatifu wa Israel. Kichwani mwake ana taji la ufalme wake: atatawala nchi toka bahari mpaka bahari, toka mto mpaka ukingoni mwa dunia.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

Sikia, Bwana ataonekana, hadanganyi hata: akikawia mngoje, kwani atafika tu, hawezi kuchelewa.
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

Bwana atashuka kama mvua juu ya ngozi yenye manyoya: katika siku zake kutakuwa na haki na amani tele; na wafalme wote wa dunia watamwa-budu, na makabila yote yatamtumikia. 
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

Mtoto atazaliwa kwa ajili yetu na ataitwa Mungu mwenye nguvu: atakalia kiti cha ezi cha Daudi baba yake; atatawala, na begani atachukua firhbo ya uwezo wake. 
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu

Ee Bethlehem, mji wa Mungu mkuu, kwako atatokea Mtawala wa Israel: na uzazi wake ni wa milele, atatukuzwa katika dunia yote; na atakapofika ita-kuwa amani humu duniani mwetu. 
K: Bwana karibu atafika, Njoni kumwabudu


ZABURI 
Mbingu ifurahi nayo dunia ishangilie,
nanyi mi-lima pigeni vigelegele. 

Milima ionyeshe furaha,
na vilima vitoe haki. 

Sababu Bwana wetu atafika,
na atawahurumia maskini wake.

Ee mbingu, nyesheni umande
na mawingu yatuletee 

Mtakatifu, nchi ifunguke
na imzae mkombozi. 

Utukumbuke, ee Bwana,
na utuletee wokovu wako. 

Ee Bwana, utuonyeshe huruma yako,
nautupe ukombozi wako. 

Ee Bwana, umlete Mwana - Kondoo mfalme wa dunia; atakayetawala toka jiwe la jangwani mpaka mlima wa binti Sion. 

Njoo utukomboe, ee Bwana, Mungu wa Majeshi: 
utuonyeshe uso wako na tutaokoka. 

Njoo, ee Bwana, utuletee amani yako: 
ili tufurahi mbele yako kwa moyo safi. 

Tupate kujua njia yako humu duniani, ee Bwana: 
na tujue wokovu wako katika makabila yote. 

Ee Bwana, amsha nguvu zako na ufike: 
ili utukomboe.

Njoo, ee Bwana, usikawie: 
uliondolee taifa lako dhambi. 

Ee, laiti ungepasua mbingu na kushuka: 
milima ingeyeyuka mbele yako. 

Njoo, ee Bwana, utuonyeshe uso wako: 
wewe unayeketi juu ya Malaika. 

Atukuzwe Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu
kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina. 


WIMBO WA BIKIRA MARIA
K: Sikilizeni, atakuja Mfalme Bwana wa dunia, naye ataondosha nira ya utumwa wetu. 

Moyo wangu wamtukuza Bwana,
Roho yangu inafurahi
kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.

Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma,
mtumishi wake mdogo,
Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu,
jina lake ni takatifu.

Huruma yake kwa watu wanaomcha
hudumu kizazi hata kizazi.

Amefanya mambo makuu kwa mkono wake:
amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;

amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, 
akawakweza wanyenyekevu.

Wenye njaa amewashibisha mema,
matajiri amewaacha waende mikono mitupu.

Amempokea Israeli mtumishi wake,
akikumbuka huruma yake.

Kama alivyowaahidia wazee wetu,
Abrahamu na uzao wake hata milele.

K: Sikilizeni, atakuja Mfalme Bwana wa dunia, naye ataondosha nira ya utumwa wetu. 

Sala: Ee Bwana twakusihi uharikishe wala usichelewe na utuletee nguvu ya juu, kusudi wote wanaotumainia huruma yako wapate kufariji wana majilio yako, unayeishi na kutawala milele. Amina.

JE, WEWE NI MDHAMBI?



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumanne, Desemba 16, 2025
Juma la 3 la Majilio


Sef 3: 1-2, 9-13;
Zab 34: 2-3, 6-7, 17-19, 23;
Mt 21: 28-32


JE, WEWE NI MDHAMBI?


Somo la leo kutoka katika kitabu cha nabii Sefania, linatoa onyo na ole kwa wale wanaokataa kusahihishwa, wanaokataa kusikia, na kuitika wito wa kumwamini Mungu. Katika somo la Injili, Yesu anasema kwamba ‘Watoza ushuru na wenye dhambi wataingia katika Ufalme wa Mungu kabla ya viongozi wa dini’. Je, ni kweli kwamba watoza ushuru na wenye dhambi waliingia katika Ufalme wa Mungu kabla ya viongozi wa dini ya Wayahudi? Je, Yesu alikuwa anasema kweli kwamba utakatifu wa watoza ushuru na makahaba ulizidi ule wa viongozi wa dini? Ndio, ilikuwa hivyo kwasababu majivuno yaliwafanya viongozi wa dini kuwa na moyo mgumu wa kupokea ujumbe wa Ufalme wa Mungu alioleta Yesu mwenyewe kwa maneno yake. Walifikiri juu ya ukubwa wao sana na walipenda wengine wawaze juu ya ukubwa wao. Walikuwa wamejiridhisha wenyewe kwa utakatifu wao wenyewe, nakujiona wema kabisa, jambo ambalo ni mbaya kweli. Lakini Yesu anayaona yote hayo, na anawanyanyua watoza ushuru na wenye dhambi kwa utayari wao wakutubu na kumpokea, Yesu anawapandisha kwenye thawabu ya Ufalme wa Mungu.

Tujitafakari sisi wenyewe kama tunamfanano na tabia ya viongozi wa dini wa Wayahudi wa kipindi hicho au tuna tabia ya hawa watoza ushuru na wenye dhambi waliokubali kupokea maneno ya Yesu. Pengine, ni vigumu kukubali. Pengine tumejitengenezea tabia ya kujitambulisha sisi wenyewe kama watu wazuri na wasio na kosa na wenye haki. Yesu anataka tujione wenyewe katika kundi hili la watoza ushuru na wenye dhambi. Hii ni kwasababu sisi wote ni wadhambi. Tunaweza tusiwe katika hali ya kuumia moyoni kama wao walivyoumia, lakini ukweli ni kwamba tunaumia kwasababu ya dhambi zetu, tunapaswa kukiri hili. Na kwakweli, kama tunashindwa kukubali dhambi zetu na madhaifu yetu, hatuna tofauti na viongozi hawa wa dini ya Kiyahudi. Tutakuwa tumebaki katika majivuno yetu na kujihesabia haki wenyewe.

Sala: Bwana, jaza moyo wangu kwa unyenyekevu. Na kwa unyenyekevu, naomba unisaidie niweze kujiona mwenyewe kama nilivyo. Nisaidie niweze kuona dhambi yangu lakini pia unisaidie kuona juhudi zangu za kukutafuta. Nisaidie niweze kuacha dhambi zangu nikurudie ili niweze kufurahia furaha na uhuru wa kuingia katika Ufalme wako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

                                    

Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, DESEMBA 16, 2025


MASOMO YA MISA, DESEMBA 16, 2025
JUMANNE, JUMA LA 3 LA MAJILIO



SOMO 1
Sef. 3:1 – 2, 9 – 13

Bwana asema: Ole wake yeye aliyeasi na kutiwa unajisi, mji wa udhalimu! Hakuitii sauti; hakukubali kurudiwa; hakumwamini Bwana; hakumkaribia Mungu wake.

Maana hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la Bwana, wamtumikie kwa nia moja. Maana toka nchi iliyo mbali na mito ya kuishi; waniombao dua, yaani, binti za watu wangu waliotawanyika, wataleta matoleo yangu.

Siku ile hutatahayarikia matendo yako yote uliyoniasi; maana hapo nitawaondoa watu wako wanaotakabari na kujivuna, wasiwe kati yako, wala hutatakabari tena katika mlima wangu mtakatifu. Lakini nitasaza ndani yako watu walioonewa na maskini nao watalitumainia jina la Bwana. Mabaki ya Israeli hawatatenda uovu, wala kusema uo0ngo; wala ulimi wa hadaa hautaonekana kinywani mwao; kwa maana watakula na kulala, wala hapana mtu atakayewaogofya.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 34:1 – 2, 5 – 6, 16 – 17, 18, 22 (K) 6

(K) Maskini aliita, Bwana akasikia.

Nitamhimidi Bwana kila wakati,
Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
Katika Bwana nafsi yangu itajisifu,
Wanyenyekevu wasikie wafurahi. (K)

Wakamwelekea macho wakati wa nuru,
Wala nyuso zao hazitaona haya.
Masikini huyu aliita, Bwana akasikia,
Akamwokoa na taabu zake zote. (K)

Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya,
Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Walilia, naye Bwana akasikia,
Akawaponya na taabu zao zote. (K)

Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo,
Na waliopondeka roho huwaokoa.
Bwana huzikomboa nafsi za watumishi wake,
Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao. (K)



SHANGILIO

Aleluya, aleluya,
Uje, Bwana, wala usikawie; Uzisamehe dhambi za taifa lako.
Aleluya.



INJILI
Mt. 21:28 – 32

Siku ile, Yesu aliwaambia wakuu wa makuhani na wazee: Mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu. Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende. Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda. Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili.

Basi yesu akawaambia, Amin, nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu. Kwa sababu Yohane alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini; nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

JE UNAKUBALI NGUVU NA MAMLAKA YA YESU?

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatatu, Desemba 15, 2025,
Juma la 3 la Majilio
 
Hes 24: 2-7, 15-17;
Zab 24: 4-9;
Mt 21: 23-27

 
JE UNAKUBALI NGUVU NA MAMLAKA YA YESU?

 
Injili ya leo inaelezea juu ya mafarakano yanayo tokea kati ya Yesu na viongozi wa dini wa wakati huo, baada ya kuwatoa wafanya biashara nje ya Hekalu (Mt 21:12-13). Mungu-Mwenyezi, katika nafsi ya Yesu Mwanae wa tangu milele yote, alikuwa akifundisha maneno ya uzima. Aliongea kwa nguvu na mamlaka na kila mtu alitambua hilo. Lakini Makuhani na Wakubwa wanaonekana wakipata hasira na wivu juu yake , huku wakimuuliza amepata wapi mamlaka? Hili swali linaonesha ni kwa jinsi ghani hawa viongozi wa dini walivyokuwa mbali na ukweli, walikuwa kipofu kabisa. Hawakufungua moyo kupokea ukweli na wala hawakuwa tayari kufungua moyo na kupokea ukombozi wa Mungu katika maisha yao. Na badala yake walisongwa na ubinafsi, majivuno na wifu. Waliogopa kama watakubali kwamba Yohane Mbatizaji na Yesu, utume wao umetoka Mbinguni, watapoteza umaarufu wao juu ya watu na watapoteza mamlaka yao juu ya watu.
 
Sisi wote tuna uongozi katika hali flani. Hata mazungumzo kati ya watu wawili, kila mtu anamamlaka flani. Kama ulikuwa kwenye hilo hekalu wakati Yesu anaongea, ungejibu nini au ungefanya nini? Je, ungemkataa? Je, ungetamani kumsikiliza zaidi? Je, utakasirishwa nae au kuwa na wivu naye? Je, utatambua nguvu yake ya Kimungu, upendo, mamlaka nakumtafuta yeye? Sisi pia wakati mwingine katika maisha yetu, tunajidanganya na kukimbia ukweli, tunataka tutawale kila kitu bila hata ya Kumruhusu Mungu afanye mabadiliko katika maisha yetu. Leo, tuamue na kukubali kupokea nguvu ya Mungu na tumruhusu yeye awe dereva wa maisha yetu katika furaha na ukamilifu wote.
 
Sala: Bwana, nisaidie kuisikia sauti yako ya utakatifu kila mahali. Nisaidie niweze kukutambua wewe kila mahali ninapoenda. Na ninapo kutafuta nisaidie nifurahi kwa kukupata wewe na kukubali yote kwa ujasiri unayosema. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
 
 

MASOMO YA MISA, DESEMBA 15, 2025




MASOMO YA MISA, DESEMBA 15, 2025
JUMATATU, JUMA LA 3 LA MAJILIO

SOMO 1

Hes 24:2-7.15-17

Siku zile Balaamu aliinua macho yake akawaona Israeli, wamekaa kabila; roho ya Mungu ikamjia. Akatunga mithali yake akasema, Balaamu macho asema, Yule mtu aliyefumbwa macho asema; asema, yeyey asikiaye maneno ya Mungu, yeye aonaye maono ya Mwenyezi, akianguka kifudifudi, amefumbulia macho; mahema yako ni mazuri namna gani, ee Yakobo, maskani zako, ee Israeli! Mfano wa bonde zimetandwa, mfano wa bustani kando yam to, mfano wa mishubiri aliyoipanda Bwana, mfano wa mierezi kando ya maji. Maji yatafurika katika ndoo zake, na mbegu zake zitakuwa katika maji mengi. Na mfalme wake atadhimishwa kuliko Agagi, na ufalme wake utatukuzwa.

Akatunga mithali yake akasema, Balaamu mwana wa Beori asema, yule mtu aliyefumbwa macho asema, yeyey asikiaye maneno ya Mungu, na kuyajua maarifa yake Aliye Juu. Yeyey aonaye maono ya Mwenyezi, akianguka kifudifudi, amefumbuliwa macho, namwona, lakini si sasa; namtazama, lakini si karibu; nyota itatokea katika Yakobo; na fimbo ya enzi itainuka katika Israeli.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 25:4 – 6, 7b – 9 (K) 4

(K) Ee Bwana unijulishe njia zako.

Ee Bwana, unijulishe njia zako,
Unifundishe mapito yako,
Uniongoze katika kweli yako,
Na kunifundisha. (K)

Ee Bwana, kumbuka rehema zako na fadhili zako,
Maana zimekuwako tokea zamani.
Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako,
Ee Bwana kwa ajili ya wema wako. (K)

Bwana yu mwema, mwenye adili,
Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
Wenye upole akawaongoza katika hukumu,
Wenye upole atawafundisha njia yake. (K)

SHANGILIO
Zab. 85:7

Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, utupe wokovu wako.
Aleluya.

INJILI
Mt. 21:23 – 27

Siku ile Yesu alipokwisha kuingia hekaluni, wakuu wa makuhani na wazee wa watu wakamwendea alipokuwa akifundisha, wakasema, Ni kwa amri gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa amri hii? Yesu akajibu, akawaambia, Na mimi nitawauliza neno moja; ambalo mkinijibu, nami nitawaaambia ni kwa amri gani ninatenda haya. Ubatizo wa Yohana ulitoka wapi? Ulitoka mbinguni, au kwa wanadamu?

Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, Tukisema, Ulitoka mbinguni, atatuambia, Mona basi hamkumwamini? Na tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, twaogopa mkutano; maana watu wote wamwona Yohana kuwa ni nabii. Wakamjibu Yesu wakasema, Hatujui. Naye akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa amri gani ninatenda haya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.